KARDINALI PREVOST ACHAGULIWA KUWA PAPA MPYA WA KWANZA M-MAREKANI
Kardinali Robert Francis Prevost, amechaguliwa kuwa Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani na kuchukua jina la Papa "Leo XIV".
.
Prevost, mwenye umri wa miaka 69, kutoka Chicago, Illinois, ndiye papa wa kwanza kabisa kutoka Marekani.
Katika maneno yake ya kwanza akiwa papa, Leo aliyeonekana mwenye hisia-moyo aliuambia umati katika Uwanja wa St. Peter “Amani iwe nanyi nyote.”
Akihutubia umati wa watu katika uwanja wa St. Peter’s Square, Leo ametoa heshima kwa marehemu papa Francis, na kuwataka umati kukumbuka urithi wa mtangulizi wake kabla ya kuelezea maono yake kwa Kanisa Katoliki.
"Tunapaswa kutafuta pamoja ili kuwa kanisa la kimisionari. Kanisa linalojenga madaraja na mazungumzo," alisema.
.
Akizungumza na maelfu ya waumini wa Kikatoliki, Leo ametoa wito kwa watu kuonyesha upendo wao kwa wengine na kuwa katika mazungumzo na upendo.
Leo alichaguliwa siku mbili tu baada ya kundi la Makadinali 133 kukusanyika katika mkutano wa kumchagua papa mpya.
Ratiba hiyo ya matukio inalingana na mikusanyiko miwili iliyotangulia, ikipendekeza kuwa Prevost aliwavutia wenzake haraka wakati wa mchakato wa usiri.
Francis na Benedict XVI wote walifunuliwa jioni ya siku ya pili ya mkutano huo, wakati John Paul II, papa aliyetawala muda mrefu zaidi wa nyakati za kisasa, alichaguliwa siku ya tatu katika 1978.
Tranding News
Newsletter
Subscribe to our newsletter to get the latest news

