SIKU YA WATOTO NJITI YAONGEZWA KWENYE KALENDA YA AFYA DUNIANI
Hatimaye, Novemba 17 imejumuishwa rasmi katika Kalenda ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kuwa Siku ya Watoto Njiti Duniani, ikiwa ni hatua muhimu ya kuhamasisha maboresho ya huduma za afya kwa mama na mtoto, hususan kwa wale wanaozaliwa kabla ya muda kamili wa miezi tisa.
Hatua hii imefanikiwa kufuatia juhudi za Mtanzania Bi. Doris Mollel, kupitia taasisi yake ya Doris Mollel Foundation ambayo kwa miaka kadhaa imekuwa mstari wa mbele kusaidia watoto njiti na kina mama nchini Tanzania.
.
Aidha, Naye Mkurugenzi Mtendaji wa WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amempongeza Bi.Doris Mollel kwa kazi yake na utetezi wa kuendeleza afya ya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati, na wao kama WHO wanatazamia kuendeleza kazi hii muhimu na ya kuokoa maisha.
Tranding News
Newsletter
Subscribe to our newsletter to get the latest news

