KIONGOZI MKUU WA IRAN ALI KHAMENEI AUAWA
Vyombo vya habari vya kimataifa vimeripoti kuwa Israel imedai Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei, amefariki dunia kufuatia mashambulizi ya anga yaliyofanyika siku ya Jumamosi.
.
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na CNN ikinukuu vyanzo viwili vya Israel vinavyofahamu tukio hilo, Israel inadaiwa kupata picha inayoonesha mwili wa Khamenei baada ya mashambulizi hayo.
.
Chanzo kingine kimeeleza kuwa tangazo rasmi kuhusu tukio hilo linaandaliwa.
.
Awali, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alisema kuna dalili nyingi zinazoashiria kuwa kiongozi huyo wa Iran “huenda hayupo tena hai.”
.
Hadi sasa, mamlaka za Iran hazijatoa tamko rasmi kuthibitisha taarifa hizo.
Tranding News
Newsletter
Subscribe to our newsletter to get the latest news

