logo

QUEEN JULIETH LUGEMBE AREJESHA FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA UBUNGO

Mwanaharakati na kada wa Chama cha ACT-Wazalendo,Bi. Queen Julieth William Lugembe leo Agosti 27,2025 amerejesha rasmi fomu ya kuwania ubunge kupitia hicho katika Jimbo la Ubungo.

‎.

‎Hatua hii inampa nafasi ya kupeperusha bendera ya chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

‎Katika tukio hilo, Bi. Queen Julieth ameambatana na viongozi wa ACT-Wazalendo, wanachama pamoja na wafuasi wake, huku akisisitiza dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Ubungo kwa uwazi, uwajibikaji na mshikamano wa kweli.

‎Aidha, Wananchi na mashabiki walijitokeza kwa wingi kumpokea na kumtakia kheri katika safari yake mpya ya kisiasa.

Frank Jordan
12345 123
Follow Us
logo

© 2023 Jordan Media. All Rights Reserved. Designed by Lylical Popcorn